gidi na ghost

Abdul alituma ujumbe  katika kituo cha utangazaji cha  Redio Jambo katika kipindi cha Patanisho ili asaidiwe kupatana na mkewe Maureen. Ndoa yao ya mwaka mmoja ilitatizika wiki iliyopita jumanne. Maureen ambaye ni bibi yake alimfumania na mke wa kakake Maureen ana madai kuwa uhusiano wao umekuwa ukifanyika kwa siri. Abdul naye anakubali na kusema alifanya hivo kimakusudi ili kulipiza kisasi.

“Alinifumania na mke wa kakake. Ilikuwa last week Tuesday tukawa tumelala. Mtu akapigia mke wangu.The next day akapiga tena saa sita usiku. Wakaanza kuongea lugha ya kwao nikakasirika nikaondokea.”

Soma hapa:

Baada ya Abdul kushuku mkewe kuwa ana jicho la nje, alianza kupatwa na wivu na kutaka pia kulipiza kisasi. Akaanza kwa ujanja kumnyemelea mke wa kaka yake Maureen.

“Shemeji alikubaliana nami basi nikasoma arafa (akafanya mapenzi naye). Tumezoea mchezo wakati nilimuulizia akakubali haraka. Ilikuwa kisasi kwa sababu huyo jamaa alisema niache kumuuliza maswali niende nimuulize bibi yangu.”

Kisasi anacholipiza kaka Abdul ni kisa na ambapo bibiye anapigiwa simu na bwana wa dadake masaa ya usiku hivo akaanza kumshuku.Kulingana na Maureen, bwana wa dadake amekuwa akimpigia kumuuliza kuhusu cheti cha kuzaliwa cha mtoto wa dadake ambaye hawaongei kwa muda.

Alipopigiwa simu na Gidi, Maureen alisema,

”Alikuwa na mke wa kakangu na huo uhusiano umedumu  kwa muda mrefu sana. Huyo jamaa anayenipigia simu usiku ni bwana ya dadangu na hatuna uhusiano na yeye. Alitaka niongee na dadangu kuhusu cheti cha mtoto. Nilipomkanya akome kunipigia simu usiku, Abdul hakuamini na akaanza kunishuku.”

Soma hapa:

Kuchepuka kwake kaka Abdul kunaonekana kuharibu ndoa hii ya mwaka mmoja kwa sababu Maureen ashatorokea kwao. Mke wake Abdul anadokeza kuwa hawapo katika mauhusiano yoyote na bwana huyu wa dadake. Anafunguka kuwa bwanake anamshuku kuwa anachepuka na mwanamme ambaye aliwahi kumuonya akome kumpigia simu usiku.

Hatimaye abdul alipata nafasi ya kusema na bibiye

“Mimi nimeona hii maisha ni ngumu kukaa peke yangu.Naomba unisamehe na turudiane.’

Bibiye hakukubali ombi lake na kusema,

“Haujui bado nikona machungu? Unatuma ujumbe kuwafurahisha wakenya ama ni mimi. Lazima utanipa muda bado nikona machungu mengi sana.”

Soma mengi pia:

Hatimaye walisameheana huku Maureen akisema kuwa ni bora waongee ili waweze kumtunza mtoto wao mchanga.

“Nitakaa nyumbani nifikirie halafu nitaona kama nitarudi baadaye,” alisema Maureen.

Kwa upande mwingine Adul alisema,

”Maureen mimi nakupenda sana. Nakuhakikishia kwamba hakuna siku nitakuplay.”

View Comments