03 June 2019 1 Min Read
Utaweza kubadilisha noti za 1000 katika benki yako –CBK
by Yusuf Juma Habari
Iwapo una noti nyingi za 1000 hautahitaji kuwa na akaunti ya benki ili kuzibadilisha na noti mpya za kisasa . Gavana wa Benki kuu Patrick Njoroge amesema utahitaji tu kutemebelea benki yoyote iliyo karibu nawe ili kuzibadilisha na noti mpya.
Hata hivyo amesema lazima anayezibadilisha notyo hizo za kale na mpya aweze kujitambulisha na kuthibitsha kwamb apesa hizo ni zake kihalali . Noti za shilingi 1000 hazitakubaliwa baada ya Oktoba tarehe moja .
Njoroge amesema wale walio na kati ya shilingi milioni moja na milioni tano za shilingi 1000 watalazimika kutremebelea benki ambazo wana akaunti ili kuzibadilisha na waeleze walivyozipata pesa hizo ili kubadilishiwa na noti mpya .