- 61196090_1362417120574999_4257206207397840919_n
- 61501565_377021072927921_6685521336903062628_n
- 62516540_2239911596094333_1537896938790832415_n

Baada ya shutuma za ukaribu na minenguo hatari kwenye fiesta ya  Choma Na Ngoma na mrembo wa Tanzania Nandy, Willy Paul ametokea kwenye kipande cha video alichochapisha kwenye mtandao wake maridhawa wa Insta. katika video hii fupi, staa huyu anaonekana na kikundi cha marafiki akijaribu kuigiza kitendo alichokifanya Askofu Ng'ang'a kanisani mwake.

"Yaani leo mnaona mnaeza mkatamani Hudda na Vera sababu nawatamani??? Lubish", anasema Willy Paul.

Kwenye kipande hicho cha video, Pozze anawatusi wanakikundi na upande mwingine wanamwogopa zaidi. Kumekuwepo na maswali mengi kumhusu muimbaji huyu wa nyimbo za injili iwapo kaasi na kubadilika kuimba nyimbo za klabu.

Pata uhondo:

Staa wa Jamaica Alaine alipozuru nchini katika tamasha kubwa iliyofanyika Kasarani ya Tomorrow's Leaders Festival alimtetea kuwa wakenya wamkosoe kwa utaratibu na upendo mwingi ili aweze kujirudi.

Mapema wiki kiongozi wa upinzani Musalia Mudavadi alionekana pia kutoa kumuonya msanii huyu. Musalia alisema kuwa wasanii wa injili wanapaswa kuwa kioo cha jamii na waonyesha mienendo ya kikristo.

https://www.instagram.com/p/Byk1hSgnOV7/

View Comments