17 June 2019 1 Min Read
Jamaa amchoma mkewe kwa kumpikia wali badala ya githeri
by Yusuf Juma Habari
Mwanamke mwenye umri wa miaka 27 anauguza majeraha katika hospitali moja ya kibinafsi huko Mwea ,Kirinyaga baada ya kuchomwa na mumewe kwa kumpikia Githeri badala ya wali .
Kwa mujibu wa shangazi yake mwathiriwa , Peter Ngugi mwenye umri wa miaka 32 alihamakishwa na hatua hiyo na kumtupia mkewe stovu iliyokuwa ikiwaka .OCPD Lucas Chebet amesema mshukiwa anasakwa ili kukamatwa na atafikishwa kortini . wawili hao wamekuwa katika ndoa kwa miaka miwili na wana watoto wawili .