- hamisa-mobetto
- hamisa.mobetto.1

Hamisa Mobetto ambaye ni mwanamitindo kutoka Tanzania amekanusha madai kwamba anadaiwa kodi. Akiongea na SnS, Mobetto, ambaye pia ni mwanamziki amesema kwamba hajawahifeli kulipa kodi ya nyumba.

"Mimi sidaiwi kodi na sijawahi kudaiwa kodi. Kila baada  ya miezi miwili huwaga wanaziongelea, kila siku nikiamka kuna habari mpya kunihusu. Mimi niko palepale na ikitokea siku ambayo nataka kuhamia sehemu nyingine, nitahama."

Mobetto ni mama wa watoto wawili. Alitamba mitandaoni alipokua kwenye uhusiano na Diamond Platnumz ambaye ni mzazi mwenza.

Hivi sasa, Mobetto anasema kwamba hayuko kwenye uhusiano wowote kwa kuwa anajishughulisha na muziki na bisahara yake ya nguo.

View Comments