04 July 2019 1 Min Read
Shinikizo la kuoa linatokana na wazazi wangu, asema Bien
by yvonne Ngugi Habari
Mwimbaji wa kikundi cha Sauti Sol, Bien asema kuwa wazazi wake wamekuwa wakimsukuma afunge ndoa.
"Wazazi wangu wamekuwa wakinishinikiza sana kufunga ndoa," Bien alisema.
Anasema wazazi wake wamekuwa wakiunga mkono kazi yake ya muziki.
Sisi ni 10 katika familia yetu na kila mtu amechagua njia tofauti, mandugu zangu wana kazi tofauti na wanafurahia kazi zao.
Bien alisema kuwa muziki umemlipia ada yake ya shule na hata kuwahamasisha wazazi wake.
Wiki tatu zilizopita, Bein aliweka picha yake na baba yake kwenye mtandao wa Instagram na kusema kuwa baba yake hakuwa na chaguo ila tu kumuunga mkono.
Bien aliendelea na kusema kuwa baba yake amekwisha kubali kuwa sitapata kazi halisi.
Watu mashuhuri kama vile Nameless walijibu kwa kusema anaonekana kushindwa juu ya utambuzi huo.