- vera
- vera.s
- vera4 (1)
- vera.s3

Inaonekana Vera Sidika amempata mwenzi wake wa maisha ambaye ni Dr Jimmy Chansa.

Vera Sidika alisema kuwa sasa yuko tayari kufunga ndoa baada ya kukutana naye mpenziwe Jimmy Chansa.

Aliendelea kusema,

Sijawahi hisi hivi kwa maisha yangu. Nataka mpenzi wangu aje akae na mimi hapa, na tuitengeneze familia na tuishi pamoja.

Aliendelea kusema kuwa Jimmy ni tofauti sana na wapenzi wake wa hapo awali kwani hajali pesa au umaarufu. Aliendelea kuongeza kuwa sasa wanazungumza juu ya mpenzi wake kuhamia Kenya.

"Kwa mara ya kwanza, nimekutana na mtu mwenye upendo na anayejali ambaye hajali pesa na umaarufu. Ana umri kama mimi. Kwa kuwa nimewekeza sana hapa Kenya, mazungumzo kati yetu ni kumfanya ahamie Kenya na aendelee kufanya mazoezi hapa. Hapo ndipo mazungumzo yetu yapo sasa, ”alifunguka.

Wawili hao walitembea huko Maasai Mara na hizi ni baadhi ya picha zao.

Soma mengi

View Comments