Jb-Masanduku-feeding-2

JB Masanduku amedai kuwa amenyimwa nafasi ya kuwaona watoto wake na aliyekuwa mkewe Tina Kagia. Kagia na Masanduku walifunga ndoa mwaka wa 2014 kwenye chemba ya Jaji.

Masanduku amesema kuwa penzi hilo lilimwadhiri hadi kwenye taaluma yake ya Muziki.

"Hii ndio sababu niliacha kufanya tasnia ya ucheshi kwani nilikosa sababu ya kuwafurahisha wengine ilihali mimi mwenyewe sina furaha." Masanduku alisema.

"Tulipeana talaka kwa amani tu na mimi namshukuru mungu kwa kuwa alikuwa na utu uzima kwenye wakati huo wote. Hata hivyo, Talaka ni jambo mbaya sana."

"Tangu tuachane sijawahi pewa ruhusa ya kuwaona watoto wangu hata mara moja ila bado mimi nawapa usaidizi wa baba. Jambo hili limenidhuru na ndio sababu nimekuwa sifanyi shoo ila nashukuru mungu kwa kuwa yeye yu mwema." Jambo hilo anasema kuwa limemwadhiri kimawazo sana  kwani hata Kagia mwenyewe hapendi kumwongelesha.

JB Masanduku amewapa ujumbe wazazi wanao wanyima waenzao nafasi ya kuwaona wanao." Mtoto atazidi kukua na akifikisha umri wa miaka 18 atakuwa na dai la kutaka kumwona babaye na hivyo atajua tu kuwa ni mamaye alimyima hio nafasi na hilo jambo sio jambo nzuri."

Pamoja na hayo, Masandukuhakutaja sababu inayomfanya Kagia kumyima nafasi ya kuwaona wanawe wawili.