Flagbearer: Mariga kupeperusha bendera ya Jubilee Kibra
Aliyekuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Harambe Stars McDonald Mariga ametangazwa kuwa mgombeaji wa chama cha Jubilee katika uchaguzi mdogo wa Kibra . Mwenyekiti wa bodi ya uchaguzi ya chama cha Jubilee Andrew Musangi amesema Mariga ndiye mgombeaji mwenye sifa tosha na uhusiano wa karibu na wakaazi wa Kibra .Mariga alikuwa katika makao makuu ya chama cha Jubilee siku ya jumatatu ili kuhojiwa na bodi ya uchaguzi na Musangi alitangaza baadaye kwamba ‘Mariga ndiye atakayekuwa sauti ya Jubilee katika eneo bunge la Kibra’. Baadhi ya masuala mabyo Mariga aliulizwa maswali kuyahusu na chama cha Jubilee ni kuhusu sera za chama hicho , iwapo anaelewa kazi ya ubunge , uwezo wa kufadhili kampeini na mpango wake wa wakaazi wa Kibra .
Bodi ya kitaifa ya Uchaguzi pia iliwahoji wagombeaji kuhusu ufahamu wa manifesto ya Jubilee na uwezo wa kuafikia maazimio yake . Jumla ya wagombeaji 16 walitaka kupewa tiketi ya chama cha Jubilee . Miongoni mwa wagombeaji hao ni Morris Peter Kinyanjui, Walter Trenk, Said Ibrahim na Doreen Wasike.Mariga sasa atamenyana na wagombeaji kutoka vyama vya ODM ,ANC na Ford Kenya katika uchaguzi huo mdogo wa Novemba tarehe 7.ODM inatarajiwa kufanya uchaguzi wake wa mchujo siku ya jumamosi baada ya kuahirisha zoezi hilo kwa ajili ya ukosefu wa usalama kwa ajili maafisa wengi wa idara za ulinzi walikuwa wakijishughulisha na sensa .ANC ilimtangaza Eliud Owalo kama mgombeaji wake kwa uchaguzi huo mdogo . Muda wa kampeini za uchaguzi huo mdogo utaanza septemba Tarehe 9 hadi Novemba tarehe 4 . Kiti hicho cha Kibra kiliachwa wazi baada ya kifo cha Ken Okoth tarehe 26 Julai mwaka huu kwa ajili ya ugonjwa Saratani .