afrika kusini

Raia wa Nigeria 640 wasajiliwa katika ubalozi wa Nigeria nchini Afrika Kusini na kundi la kwanza la raia hao litaondoshwa Jumatano kufuatia mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.

Ndege ya Air Peace itaondoka Johannesburg saa tatu kamili asubuhi kwa saa za Afrika Kusini na inatarajiwa kuwasili mjini Lagos kwa saa za Nigeria.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya nchi za nje ya Nigeria kwenye ukurasa wake wa twitter inakadiriwa kuwa idadi ya raia 313 watachukuliwa kutoka Afrika Kusini katika awamu ya kwanza na waliosalia watasafirishwa siku za Alhamisi na Ijumaa wiki hii.