- DORN
- ANACLET (1)
- dorn (1)

Dorn Anaclet, kijana ambaye ana miaka 26 akiwa mmoja wa wagombea wa kiti ya ubunge ya Kibra. Dorn anawania kiti hicho na chama cha Democratic ambacho ni cha aliyekuwa Rais wa tatu wa jamhuri ya Kenya, Mwai Kibaki.

Dorn ama "kijana mdogo" kama jina wafuasi wake wanavyopenda kumuita, ni mchanga, hajuani mtu yeyote au kuwa na 'baba wa kisiasa' tofauti na washindani wake wenye uzoefu kubwa zaidi.

Dorn huwa anafanya kampeni zake kila siku kwa miguu chini ya jua kali la Kibra akiuza manifesto yake kwa wenyeji wa mtaa huo. Yeye anapenda kuwafikia wafuasi wake kwa miguu ili kuwatambua vyema wapigaji kura, kwani huo ndio uwezo wake.

Maisha ya Dorn yalijawa na msururu wa bahati mbaya.
Alipoteza wazazi wake mnamo 2005 akiwa na umri wa miaka 12. Alipofikisha miaka 13, aliondoka Homabay kuenda Nairobi kujaribu bahati yake maishani.
Aliishi katika makazi duni Kibra ambayo anasema yalikuwa na watu wengi kutoka kabila lake ya Luo. Dorn alianza safari ya elimu baada ya kusaidiwa na msamaria mwema huku akifanya vizuri katika mitihani yake.
Alisomea katika shule ya upili ya Orero kabla ya kujiunga na chuo kikuu cha Nairobi, ambapo alisomea shahada ya sanaa katika uchumi na sayansi na alihitimu mwaka wa 2016. Hivi sasa anasomea shahada ya uzamili katika ukuzaji wa kimataifa katika chuo kikuu cha Nairobi.

Dorn pia amewahi kuwa kiongozi katika chuo kikuu cha Nairobi huku akichaguliwa mara tatu kutumika katika vyeo tofauti ndani ya SONU.

Manifesto ya Dorn imejikita katika nguzo tatu, elimu, maji, na mazingira safi.