09 October 2019 1 Min Read
Siri ni ipi? Tanasha Dona aonyesha mwili wake baada ya kujifungua
by sedellar righa Habari
Kwa kweli, nimeshindwa kuamini macho yangu baada ya kuona picha za kidosho huyu.
Siamini kwamba binti huyu, mpenziwe Diamond alijifungua kitoto kichanga wiki iliyopita na kwa sasa anafanana hivi.
Tanasha Dona aliweka picha zake kwenye mtandao wa kijamii si moja bali picha mbili akionyesha wazi vile ambavyo mwili wake unafanana pindi tu baada ya kujifungua.
Kina mama wengi hupitia makuu wakijaribu kupunguza ufuta ukujao baada ya kujifungua lakini ni kama vile Tanasha hakupitia makuu hayo.
Hebu tazama picha za mrembo huyu baada ya kujifungua.
Aisee, ni wazi bayana kuwa kuna mabinti walioumbwa wakaumbika.