Jam Ngara

Magari manane Alhamisi asubuhi yalihusishwa katika ajali ya barabara ya Thika katika eneo la Kituo cha Polisi cha Muthaiga.

Ajali hiyo mwanzo ilisababishwa na mabasi mawili ya kampuni ya Virginia Coach na basi la Mwiki Sacco kabla ya magari mengine kuhusishwa.

Kamanda wa polisi katika kaunti ya Nairobi Philip Ndolo amesema kwamba basi la kampuni ya Virgnia iliteleza na kugonga  vichuma kando kando mwa barabara telezi kutokana na mvua kubwa unaonyesha.