Mwanaume ashtakiwa kwa kuuma sehemu nyeti za mwanawe
Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 23 huko Voi, kaunti ya Taita Taveta amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumuuma na kumkata uume wake mwanawe mwenye umri wa miezi minne.
Hayo yakijiri, wananchi kutoka eneo la Changara kaunti ndogo ya Teso kaskazini kaunti ya Busia wamejitokeza kulalamikia kusitishwa kwa mradi wa ujenzi wa bwawa eneo hilo wa kima cha shilingi milioni 24.
Wakizungumza na wanahabari katika soko la Changara, wananchi hao wameelezea umuhimu wa mradi huo kwa jamii ikizingatiwa kuwa wenyeji wa eneo hili wamekuwa wakihangaika kutafuta maji.
Hata hivyo mwanakandarasi huyo Cleophas Mamai amesisitiza kuwa sharti matakwa yake yatimizwe ikiwemo kubuniwa kwa kamati ya kusimamaia mradi, matakwambayo wananchi wanasema yametimizwa huku wakimshutumu mwanaharakati huyo kwa kulemaza mendeleo katika eneo hilo.