Rais mstaafu Daniel Toroitich Arap Moi hatimaye ameondoka kutoka Nairobi Hospital alikokuwa akitibiwa baada ya kupata nafuu.

Kikosi cha utabibu wake kinaongozwa na daktari David Silverstein aliidhinisha kuwa Mzee Moi yu nafuu kiasi cha kuruhusiwa kuondoka hospitalini

"Familia ya Moi inawashukuru wale wote waliomwombea na kumtakia nafuu ya haraka," katibu wa kibinfasi wa  Moi Lee Njiru alisema Alhamisi.