Mbusii atuzwa tuzo ya mtangazaji bora barani Afrika, Gidi ampongeza
Mtangazaji Mbusii ametwaa ushindi mkubwa nchi ya Ghana baada ya kushinda tuzo ya kipengele cha mtangazaji bora Afrika.
Mashindano haya yanahusisha mastaa wa redio Afrika kati ya miaka 18-35 wanaoaminika kuwa na mchango mkubwa katika jamii wanayoishi.
Baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Mbusii hakuweza kuficha furaha yake.
https://www.instagram.com/p/B5UhzcSAYRl/
"Nashukuru Mungu. Ushindi ni wetu wakenya. Nashukuru kila mtu kwa maombi..." Alichapisha Insta.
Watangazaji Gidi, Maina na wengineo pia wamempa kongole kwa kupata tuzo hiyo,
"Heshima kubwa sana kwako Mbusii. Ahsante kwa kuipeperusha bendera ya Kenya juu zaidi kutoka. Enyewe wewe na Lion ni miongoni mwa watangazaji waliojaliwa kipaji kikubwa," Alichapisha Maina.
"Pongezi sana kwa Tuzo la the Radio personality 2019 35.35 Africa awards winner 👆👆🙏👏 Wagwan," Alichapisha Gidi Insta.
https://www.instagram.com/p/B5Ta5V9pOrX/