Matokeo ya KCSE: Idadi ya wanafunzi waliopata alama ya 'A' yaongezeka
Jumla ya wanafunzi 627 walijizolea alama ya 'A' katika mtihani wa mwaka huu wa KCSE, kutoka 315 mwaka jana, waziri wa elimu George Magoha amesema.
Baraza wa shule ya upili ya Kenya High alijizolea gredi A yenye alama 87.087.
Kaboge Odhiambo kutoka shule ya upili ya Kapsabet alipata gredi A na alama 87.080, Antony Owuor alipata A ya alama 87; Natasha Wawira wa Kenya High alipata gredi ya A ya alama 86.9.
"Matokeo yanaonyesha uboreshaji mkubwa ukilinganisha na yaliyoshuhudiwa katika miaka mitatu. Walimu wetu wanawashirikisha watahiniwa bora. Kwa hivyo naweza kusema hakukuwa na wizi wa mtihani," Magoha alisema.
Idadi ya watahiniwa 125, 746 walijizolea alama ya C+. 2018 idadi ya watahiniwa 96,377 ndio waliojizolea C+.
Jumla ya wanafunzi 699,745 walifanya mtihani wa KCSE mwaka huu ambao ulikamilika November 27.
Mwaka uliopita, Juliet Otieno kutoka shule ya upili ya Pangani ndiye aliyeongoza baada ya kujizolea alama 87.6, huku akifuatwa kwa karibu na Kaluna James wa chuo kikuu cha Maseno na alama 87.3.