29 December 2019 1 Min Read
Orodha ya wagombea wa viti mbalimbali ambao hawakujipigia kura wakati wa uchaguzi
by Abel Omasete Habari
- mariga
- sifuna
- dona
- mariga-kibra
Hawa ni baadhi ya watu ama viongozi ambao walijitosa uwanjani kugombea katika viti mbali mbali humu nchini katika uchaguzi, na hawakuweza kujipigia kura katika eneo hilo ambalo walikuwa wanagombea, kisa na sababu hawakujisajili kama wapiga kura katika eneo hilo.
1. Mc Donald Mariga
Alikuwa mchezaji wa timu ya taifa Harambee stars na leo hii hakuweza kujipigia kura katika uchaguzi mdogo unaoendelea katika eneobunge la Kibra akiwa anagombea kiti hicho kupitia tikiti ya chama cha Jubilee.
Tume ya kusimamia uchaguzi nchini IEBC ilithibitihsa kuwa Mariga hajajisajili kupigia kura katika eneobunge hilo.
2. Edwin Sifuna
Sifuna ambaye ni katibu katika chama cha ODM aligombea kiti ya useneta jijini Nairobi mwaka wa 2013 kupitia chama cha ODM huku ushindani mkubwa ukishuhudiwa kati yake na Johnson Sakaja wa chama cha Jubilee.
Sifuna ambaye alijisajili kama mpiga kura katika kaunti ya Bungoma kule Kanduyi hakuweza kujipigia kura katika kinyang'anyiro hicho.