- mariga
- sifuna
- dona
- mariga-kibra

Hawa ni baadhi ya watu ama  viongozi ambao walijitosa uwanjani kugombea katika viti mbali mbali humu nchini katika uchaguzi, na hawakuweza kujipigia kura katika eneo hilo ambalo walikuwa wanagombea, kisa na sababu hawakujisajili kama wapiga kura katika eneo hilo.

1. Mc Donald Mariga

Alikuwa mchezaji wa timu ya taifa Harambee stars na leo hii hakuweza kujipigia kura katika uchaguzi mdogo unaoendelea katika eneobunge la Kibra akiwa anagombea kiti hicho kupitia tikiti ya chama cha Jubilee.

 Tume ya kusimamia uchaguzi nchini IEBC ilithibitihsa kuwa Mariga hajajisajili kupigia kura katika eneobunge hilo.

2. Edwin Sifuna

Sifuna ambaye ni katibu katika chama cha ODM aligombea kiti ya useneta jijini Nairobi mwaka wa 2013  kupitia chama cha ODM  huku ushindani mkubwa ukishuhudiwa kati yake na Johnson Sakaja wa chama cha Jubilee.

 Sifuna ambaye alijisajili kama mpiga kura katika kaunti ya Bungoma kule Kanduyi hakuweza kujipigia kura katika kinyang'anyiro hicho.

View Comments