PAMBANA NA HALI YAKO! Wakenya mtandaoni wamkemea Dennis Itumbi baada ya kushambuliwa na polisi
‘The Internet never forgets’- Ni kauli ambayo umeisikia mara kadhaa hususan katika matukio ambayo mtu anasema kitu wakati Fulani bila kujua kwamba sikumoja atajutia .Ndio masaibu yaliomfika Dennis Itumbi alipoweka video mtandaoni akilalamika jinsi polisi 18 walivyomshambulia na kumpa kichapo bila huruma katika kituo cha polisi cha Kilimani siku ya Ijumaa tarehe 10. Itumbi anasema alikuwa amekwenda kulichukua gari lake wakati polisi walipomvamia .
“Wamenichapa, wamenishambulia kweli .yaani polisi 18 wamenipiga makonde …hawa ni watu aina gani ?’“ Kosa langu lilikuwa kwenda katika kituo cha polisi kuchukua gari langu’ alisema Itumbi .
Lakini watumiaji wa mitandao waliichakura na kutoa ujumbe ambao Itumbi aliuandika mwaka wa 2016 uliosema :‘ Sheria inawaruhusu polisi kutumianguvu katika hali Fulani na mahakama kote ulimwenguni zinatambua hilo’. Itumbi alindika ujumbe huo Mei tarehe 23 mwaka wa 2016 .
Masaibu yake hayo yalijiri saa chache tu baada ya mbunge wa Gatundu Kusini moses Kuria pia kukamatwa katika kituo hicho cha polisi kwa kumshabulia mwanadada mmoja .Kupitia akaunti yake ya Twitter Itumbi alisema alifanyiwa matibabu na alikuwa tayari kurejea katika kituo hicho kuhakikisha kwamba Kuria anaachiliwa huru .