20 January 2020 1 Min Read
ROGUE BLOGGER:Mwanablogu Cyprian Nyakundi akamatwa kwa hila ya kupunja shilingi Milioni 17 kutumia vitisho
by Yusuf Juma Habari
Makachero wamemkamata mwanablogu Cyprian Nyakundi na mshukiwa mwingine Emmanuel Nyamweya Ong'era kwa njama ya kutaka kupokea shilingi milioni 17 ili kuondoa chapisho la mtandaoni la kumharibia mtu jina .
Wawili hao tayari walikuwa wameshapokea shilingi milioni 1 kama sehemu ya malipo hayo .
https://twitter.com/DCI_Kenya/status/1219238606184894464
Inadaiwa wawili hao waliitisha kiasi hicho cha pesa kama sharti la kuondoa chapisho hilo kutoka kwa blogu inayomilikiwa na Nyakundi . wawili hao watazuiliwa na polisi hadi Jumanne tarehe 21 watakapofikishwa kortini . Pesa hizo pia zilipatikana na zitatumiwa kama ushahidi .