SUTI ZA MWILI WA MOI :Mwili wa Mzee wavalishwa suti tofauti kila siku unapotazamwa .
Mwili wa marehemu Mzee Daniel Moi ulivalishwa suti tofauti kila siku ambayo ulipelekwa bungeni kutazamwa na wananchi .
Siku ya jumatatu ambayo ndio ya mwisho mwili huo kuwekwa katika majengo ya bunge ili kutazamwa na umma , mwili wa Moi ulivalishwa suti ya rangi ya kijivu (grey) ,viatu vya rangi ya kahawia(brown) ,shati jeupe na tai yenye vistari vya manjano . Kirungu kidogo cha mzee Moi al maarufu fimbo ya nyayo kiliwekwa katika mkono wake wa kulia kinyume na siku mbili za awali ambapo kiliwekwa kando yake . Siku ya kwanza ya kuutazama mwili huo jumaosi ,ulivalishwa suti ya rangi ya kijivu shati jeupe na viatu vya rangi ya kahawia na tai yenye maua . Siku ya jumapili iliyokuwa ya pili kwa mwili wake kutazamwa na umma ,alivalishwa suti nyeusi ,shati jeupe ,tai ya rangi nyekundu na viatu vyeusi .
Viongozi ambao tayari wameuona mwili wa Mzee Moi ni pamoja na rais Uhuru Kenyatta ,naibu wake William Ruto ,rais mstaafu Mwai Kibaki ,mabalozi ,wabunge na maseneta,magavana na viongozi wa kidini .
Rais huyo wa zamani atapewa taadhima zote za kijeshi wakati wa maazishi yake ikiwemo saluti ya milio 19 ya risasi . Siku ya jumanne misa ya madhehebu mbali mbali itafanyika katika uwanja wa Nyayo Nairobi . Moi atazikwa nyumbani kwake Kabarak siku ya jumatano .