Jamaa mmoja yuko kwenye njia panda sasa hivi baada ya kufichua kuwa kuna mwanadada ambaye alipachika mimba licha kuwa na mke.

Anasema kuwa mkewe alikuwa anaishi Ruiru naye alikuwa anaishi Rongai. Siku moja alialika mwanadada kwa nyumba baada ya kumuahidi kumfanyia sherehe ya kusherehekea birthday.

Wawili hao walishiriki ngono na ilipofika siku ya kuondoka, yule mwanadada kwa jina alibeba radio na televisheni.

Baada ya miezi kadhaa yule Faith alimpigia simu akimuarifu kuwa yeye ni mja mzito na anataka kuanza kuishi naye. Je atafanyaje?

Soma usimulizi wake,

Ilikuwa last year mwezi wa tisa na mke wangu alikuwa anafanya kazi Ruiru, nami naishi Rongai. Sasa kuna msichana tulikuwa tuna chat naye Facebook, nikampee number yangu tukaanza ku chat.

Sasa huyu msichana kuna siku aliniambia ako na birthday na alitaka nimfanyie party. Nikamwalika kwangu bibi yangu akiwa job na akaja akakaa huku siku mbili na siku ya tatu tukafanya birthday.

Alienda kesho yake nami nikaenda job na nilipata amebeba TV na woofer yangu ameenda nazo, na wakati nilimpigia simu akaniambia niwache kumsumbua.

Baada ya mwezi moja unusu akanipigia simu akisema akona ball yangu. Siri natka imtobokee bibi yangu nimwambie kuna msichana alienda na TV, woofer na ball yangu. Huyo msichana anaitwa Faith.

Kuna watu walipigia mke wangu simu wakimwambia wameona mwanadada kwangu na nikamdanganya alikuwa cousin yangu.

Ubaya ni eti mke wangu sasa tunaishi pamoja Rongai na huyu anataka pia kuja kuishi na mimi. Isitoshe mke wangu naye ana ball pia.

View Comments