Fire Moto! Jumbe za mapenzi kati ya gavana Lonyangapuo na mpenzi wake zalipuka
Mpenzi wa gavana wa West Pokot John Lonyangapuo amevuja jumbe zao za mapenzi mtandaoni .
Radio Jambo imepata jumbe na picha hizo za mawasiliano kati ya Lonya na kipenzi chake .
Katika mawasiliano hayo ya whatsapp ,mpenzi huyo anaahidi kumzalia mheshimiwa mtoto wa kiume . Gavana ambaye amejawa sana na furaha anajibu ;
“WONDERFUL.”
Kisha mheshimiwa anazidi kwa kuandika ujumbe huu wa mapenzi
“I LOVE YOU CHEMANENYU.”
Anafuatisha ujumbe huo kwa picha yake ya selfie na kisha kupiga busu ya hewa .
Katika picha hiyo ya selfie ,Lonya amevalia vesti ya rangi nyeupe huku akiupisha miomo yake kwa busu .
Mazungumzo yanatamatika wakati mwanamke huyo anaposema kwamba ;
“mzee is around”.
Kisha anaahidi kusema naye zaidi keshoye . Gavana Lonyangapuo hajazungumzia mlipuko wa jumbe hizo .
Zicheki hapa