MC-Jessy-smiling

NA NICKSON TOSI

Joe Muchiri ameibua hisia mitandaoni baada ya kutuma video iliyokuwa inawaonyesha MC Jessy na Betty Kyallo usiku wakiwa katika kituo cha kuuza  petroli.

Katika video hiyo Joe anasikika akimuuliza MC Jessy maswali kuhusiana na hatua ya wawili hao kuwa nje usiku wakati ambapo serikali ilikuwa imetoa onyo kwa wananchi dhidi ya kuzurura kuhusiana na mkurupuko wa virusi vya Corono.

busted 😜 @jessythemc jana ame sema watu wakae home na Nime mpata hapa Lenana road aki tangatanga 🤷🏾‍♂️🤷🏾‍♂️ muache double standards Corona is not spread at night only iko hata mchana, mna penda ku ingilia watu wa #UsikuSacco coz wanaraha mingi kuwa shinda 🙂😜 Hata Hio asteroid inakuja kuanguka mta sema ni sisi tumeleta 😒😒 Acha niingie CBD  😴😴 #StayHome24/7 aliandika Joe.

Japo kile  kilichonadi macho ya wengi ni uwepo wa Betty na Jessy katika eneo moja swala lililoibua maswali mengi ya iwapo ni msomali aliyekuwa anasemekana kuwa anamchumbia mwanahabari wiki chache zilizopita.Betty alikuwa anatuma picha za msomali huyo katika mitandao yake ya Instagram kila mara japo uhusiano wake na MC Jessy umeibua hisia kinzani miongoni mwa wakenya.

Video aliyotuma Joe Muchiri ndio hii hapa