Jesso!!Mkewe Alikiba awashangaza wengi baada ya kuposti video ya wabeba jeneza
Mkewe mwanamuziki wa nyimbo za Bongo Alikiba Amina Khalef aliwaacha wengi midomo wazi na maswali chungu nzima kama kila kitu kiko sawa katika maisha yake.
Hii ni baada ya kuposti video katika mtandao wa kijamii wa wanaume wakiwa wamebeba jeneza au sanduku la maiti, wanaume hao kutoka Ghana wameenea sana katika mitandao ya kijamii kwa kazi wanayofanya.
"R.I.Pπ." Aliandika ujumbe mfupi baada ya video hiyo.
Wabeba jeneza hao huwa wanalipwa kubeba maiti ili kuwapa safari njema huku wakicheza mziki.
Mashabiki wake kwa haraka walitoa hisia zao kuhusiana na video hiyo huku wengi wakisema kuwa si kwema. Uhusiano wa Alikiba na Amina umekuwa na uvumi mwingi kuwa wameachana.
jumalokole2 πππππππ nilizani pambe ni kwangu tu πππππ kumbe adi kwa mke wa YOOOOOO πππππ kawapost wazee wa kazi wanaenda kuzika ππππ leo kucheleeeeeeeee
vee.24 Makaburi ya mombasa yamedamshi leo wanataka wakazikie kariakoo
mamush_mamuh ππππbado biriani tu msiba kwisha
imani_amani Kwisha maneno, Amina na Tanasha msirudi nyuma aiseeπ
sirimsambya Humo kuna adi vyeti vya ndoa π
kenerd_di_blackmoon Nini tena, usiwe umezika ndoa humu duh tutaambia nn watu
Akimjibu mmoja wa mashabiki aliyemuuliza kwamba atarudi nchini Tanzania lini kwa maana sasa Amina anaishi na wazazi wake mjini Mombasa alikuwa na haya ya kumjibu.
"I LOVE TANZANIA AND WILL COME VERY SOON." Amina Alisema.