Vera Sidika Unapenda watu wangapi? Baada ya kuachana na Chansa Vera sasa asema anampenda Xtian Dela
Miezi tu baada ya kuachana na mpenzi wake wa Tanzania Chansa,Vera Sidika sasa amemuangazia mwanamitandao Xtian Dela.
Vera amekuwa na msururu wa wanaume katika maisha yake na alianza uhusiano na Chansa baada ya kuachana na Otile Brown .
Akiandika kwenye instagram,Vera alisema ;
“XTIAN IS MY HOMIE IN CASE YOU DIDN’T KNOW. HE ACTUALLY INCITED ME TO START A LIVE SHOW BTW, SIN CITY AND I THINK HE IS A GOOD LOOKING GUY.
I EVEN TOLD HIM THIS. I LOVE YOU XTAIN DELA,”
Xtian Dela alishangazwa na ufichuzi huo na kuandika
“WUEH! THIS IS THE SECOND ‘I LOVE YOU’. EBU DROP YOUR PIN AND SEE. I ALSO HAVE A MEDIA PASS FOR CURFEW HOURS. ESPECIALLY THE WAY YOU ARE MARINATED.”
Baada ya kugundua alichofanya Vera alianza kulaumu maandishi yake kwa sababu ya ‘ulevi’. Na tunavyojua hakuna mtu mkweli kama mlevi . Ingawaje penzi halifichiki, wengi walishangaa iwapo yeye na Dela hata wanawiana kwa karibu.
Akilinganishwa na Chansa, Xtian ni kama ‘contractor’ –unampa kibarua cha siku tu kisha unamuachilia aendelee na maisha yake.