Rais Uhuru Kenyatta ametangaza kwamba Kenya itawaajiri wafanyikazi  5000 zaidi wa afya .

Watakaoajiriwa ni walio na  stashahada (Diploma) na Astashahada (Certificate).Akilihutubia taifa akiwa Ikuli siku ya jummaosi  amesema wafanyikazi hao watahudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja .

Amesema  shilingi bilioni 1.7 zitatengewa hospitali  za umma kuongeza idadi ya vitanda vya wagonjwa . rais Uhuru ameongeza kwamba  serikali itatenga raslimali zaidi kwa taasisi za utafiti .

"... Ili kufanikisha ubunifu mpya  wa kutusaidia kukabiliana na coronavirus’ amesema

Rais Uhuru Kenyatta  alikuwa akiratibu   mikakati ambayo serikali imechukua ili kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia mpango wa kuzifadhili sekta mbali mbali  wakati huu taifa linapokabiliana na janga la virusi vya corona . Wakati wa hotuba yake alitangaza pia kwamba kuna visa vipya 31  vya watu walioambukizwa virusi vya corona  na kufikisha idadi hiyo kuwa 1,192.

Wiki jana madaktari walieleza hofu yao ya kucheleweshwa kwa  mpango wa kuwaajiri  wafanyikazi wa ziada  katika sekta ya afya licha ya ongezeko la idadi ya wagonjwa wa Covid 19 .

View Comments