USHURU-TUSKER

Klabu inayoshiriki ligi kuu ya divisheni ya pili nchini Kenya Ushuru imewatimua wachezaji 20 kama njia ya maandalizi katika msimu mpya wa 2020/2021.

Walipaji ushuru hao wamekuwa wakipigania nafasi ya kurejea kwenye ligi kuu ya KPL tangu washushwe ngazi mwaka 2016 na walimaliza katika nafasi ya 16 na alama 26 kutoka kwa mechi 30..

Miongoni mwa wachezaji walioonyeshwa mlango ni kama  Edwin Mwaura, Bonface Barasa, John Ndirangu, na Bonface Makhacha amongst na wengine wengi.

“We regret to inform you that we will be ending your term of employment with us as from July 1, 2020,” ni taarifa iliyotoka kwenye klabu hiyo.

Kulingana na barua hiyo ,iliandikwa Mei 29 na kutiwa saini na mkurugenzi mkuu wa Ushuru Stephen Mathenge..

“Please consider the aforementioned date as your last day of work. This is done in compliance with the minimum notice period required by your contract,”inasema barua hiyo.

Mechi za humu nchini ikiwemo ligi kuu ya KPL ilisitishwa kutokana na janga la corona.