ufFuCdPa.jfif

Viongozi kutoka eneo la Magharibi wameapa kuendeleza umoja wa jamii ya eneo hilo kuhakikisha wakazi wanatimiziwa mipango ya maendeleo.

Wakiongozwa na Kinara wa chama cha Ford Kenya Moses Wetang'ula,  Spika wa Seneti Ken Lusaka, viongozi hao walisema hawatakubali kugawanywa kwa misingi ya kisiasa na watu ambao wana tamaa za kibinafsi.

Wabunge Alfred Agoi (Sabatia), Chris Wamalwa (Kiminini), Omboko Milemba (Emuhaya) na wengineo walisema jamii ya Waluhya inawatambua seneta Moses Wetnagula na na mwenzake wa ANC Moses Mudavadi kama wasemaji wa jamii ya Mulembe.

Kwenye hotuba yake Wetang'ula ambaye pia ni seneta wa Bungoma alielezea hofu yake huenda taifa likarejea kwenye mfumo wa chama kimoja iwapo serikali na taasisi husika hazitalinda matunda ya kidemokrasia.

Viongozi hao walizungumza kwenye mazishi ya mama wa mbunge wa Luanda Chris Omulele, kaunti ya Vihiga.

Mamake Omulele, Sophia Monyo aliaga dunia Ijumaa, Juni 2020.