wEFk9kpTURBXy84OThhYjAwNDgwODVjZTZjNzY1NDQ5ZDg1M2I2YmY3YS5qcGeRkwXNAxTNAbyBoTAB

Naibu Rais William Ruto alhamisi alipatana na seremala waliovuma mitandaoni hivi majuzi kwa ajili ya benchi ya meza nyumbani kwake katika eneo la Karen.

Ruto aliposti mazungumzo yao na seremala hao Stephen Odhiambo na Dennis Otieno kwa kazi yaao nzuri iliosababisha wasambae sana kwenye mitando ya kijamii siku chache zilizopita.

"I was privileged to meet and interact with Stephen Odhiambo and Dennis Otieno, two enterprising Kenyans with innovative ideas on garden furniture. I was thrilled by their cutting-edge skills and efforts." Alizungumza Ruto.

Naibu rais aliagiza benchi tofauti huku akifanya mazungumzo kuhusu bei ya benchi hizo na seremala hao ili wamuuze kwa bei nafuu.

"Have a field around here and I need three more units, how much would you charge me for the three? Sh100,000?" Ruto Aliuliza.

https://twitter.com/WilliamsRuto/status/1276226630554353664

Seremala hao walimuuzia kila benchi kwa shillingi 50,000, alizidi kujadiliana nao na kuwaabia wanapaswa kufikiria kuhusu hustler au mfanyabiashara mwenzao.

"Please you have to consider your fellow hustler, you can't charge me that whole money. What would you charge rich people if you want to charge me Sh50,000 for one?"

Baadae walikubaliana beei na kuweka siku ya kumpelekea naibu benchi hizo.

View Comments