01 July 2020 1 Min Read
Matiang'i: Kenya iko tayari kurejelea usafiri ndani nan je ya nchi
by Yusuf Juma Habari
Vikwazo vya usafiri huenda vikaondolewa na serikali baada ya uzinduzi wa mwongozo wa taratibu za utalii ,afya na usalama .
Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang'i amesema taifa sasa lipo salama kwa usafiri . Matiang’I amesema serikali itazidi kuimarisha usalama na kusimamia shughuli zote za uangalizi ili kuzuia maambukizi zaidi ya virusi vya corona .
Amesema hali ilivyo sasa itawalazimu wakenya kujifunza kuishi na virusi vya corona huku juhudi za ulimwengu mzima kutafuta tiba zikiendelea .
Kauli yake hiyo imekaririwa pia na waziri wa Afya Mutahi Kagwe.serikali ilisitisha usafiri wa aina yoyote wa kimataifa mwezi aprili ili kuthibiti maambukizi ya covid 19 .