Watu 3 wakamatwa kwa utekaji nyara na kuitisha fidia ya shilingi 150,000 Meru
Watu watatu wamekamatwa kwa utekaji nyara na kitisha fidia ya shilingi elfu 150 ili kumuachilia mateka wao huko Meru .
Patrick Kimathi, Joseph Karithi na Daniel Muroki wote walio na umri wa chini ya miaka 30 walikamatwa baada ya ripoti ya mtu aluyepotea kuwasilishwa kwa polisi .
Maafisa wa DCI wamesema ripoti hiyo ilikuwa imewasilishwa kwa kituo cha polisi cha Kangeta ,Meru juni tarehe 19 mwaka huu .
Makachero kwa ushirikiana na polisi kisha walianza oparesheni iliyopigwa jeki na habari za ujasusi katika eneo la Kiutune ,Igembe ya kati . Polisi hao walielekezwa katika msitu wa Njuri Ncheke katika kijiji cha mpinda ambako washukiwa walionekana wakijaribu kutoroka lakini wakakamatwa kwa usaidizi wa wananchi .
Watatu hao kisha waliwaelkeza polisi katika kichaka kilichokuwa karibu ambapo mateka wao aliokolewa baada ya kuzuiliwa katika eneo hilo kwa siku 14 .
Mwathiriwa alipelekwa hospitalini kwa uangalizi huku washukiwa wakizuiliwa na polisi na vitu kadhaa kuchukuliwa katika eneo la uhalifu ili kutumiwa kama ushahidi .