13 July 2020 1 Min Read
Tanzia: Bintiye shujaa Nelson Mandela, Zindzi aaga dunia
by Grace Muia Habari
Bintiye aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela ameaga dunia akiwa kwenye hospitali ya Johannesburg alipokuwa anapokea matibabu.
Zindzi, 59, alihusika katika vita vya kupata uhuru nchini Afrika Kusini. Mama yake, Winnie Mandela ambaye pia ni marehemu aliwacha historia ya kupambana kumaliza ubaguzi wa rangi nchini humo.
https://twitter.com/Siseko_Soga/status/1282552683405217794
Kabla ya kifo chake, Zindzi alihudmu kama balozi wa Afrika Kusini nchini Denmark.