Aibu gani? OCS Miongoni mwa waliokamatwa kwa kuiba pombe Kisumu
OCS wa kituo cha polisi cha Boya huko Kisumu chief inspector William Cheruiyot ni miongoni mwa maafisa wa polisi waliokamatwa siku ya jumatatu kwa kuiba pombe .
Afisa huyo alikamatwa pamoja na wado wake wanne Jane Chepkemei (CP No. 83816), Bernard Macharia ( PC No.110581), Samuel Maina ( PC No.119196) na Rodrick Laushuset (PC No. 59664).
Ripoti ya polisi inaonyesha kwamba walikamatwa baada ya kuiba pombe ya White Pearl Vodka kutoka kwa lori ambalo lilipata ajali wakati lilipokuwa likisafirisha pombe hiyo . Ajali hiyo iliyohusisha lori la Isuzu KCK 959L haikusababisha majeraha ya waliokuwemo .
Polisi hao wanadaiwa kuiba pombe hiyo badala ya kuilinda na baadaye chupa 72 za kileo hicho zilipatikana katika nyumba ya OCS Cheruiyot .
Tukio hilo liliripotiwa katika kituo cha polisi cha Ahero ,kaunti ndogo ya Nyando kupitia nambari ya OB OB3/10/08/2020 NA 41/10/2020.
OCS huyo alizuiliwa katika kituo cha polisi cha Kisumu Central .