Tanzania  imeondoa marufuku  dhidi ya safari za ndege za Kenya nchini humo siku moja tu baada ya Kenya  kuwaruhusu raia wa Tanzania kuja Kenya bila kuhitajika kwenda karantini ya lazima  ya siku 14 .

Kupitia taarifa  iliyotolewa jumatano  mkurugenzi mkuu wa maamlaka ya safari za ndege nchini Tanzania Hamza Johari amesema safari zote za ndege kutoka Kenya sasa zinaruhisiwa katika anga ya Tanzania .

Kenya siku ya jumanne iliamua kuiweka Tanzania katika rodha ya mataifa ambayo raia wake sio lazima wawekwe katika karantini ya siku 14 wanapowasili nchini . Mataifa mengine yaliwekwa katika orodha hiyo ni pamoja na  Ghana, Nigeria na Sierra Leone.

Mwezi agosti Tanzania  ilipiga marufuku shirika la Kenya Airways dhidi ya kwenda nchini humo na kuzidisha mgogoro kati ya nchi hizo mbili

 

View Comments