In Summary
  • Wakenya milioni 3.1 wanaunga mkono mswada wa BBI mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati asema
  • Kaunti 12 kati ya 47 wamepitisha mswada huo

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka imetangaza jumla ya saini za BBI milioni 3.18 zimethibitishwa wakati inahitimisha zoezi hilo.

Hii ni nje ya saini milioni 4.3 zilizokusanywa na timu ya BBI mwaka jana.

IEBC ilihitaji tu kuthibitisha saini milioni moja ili Mswada wa BBI upelekwe kwa mabunge 47 ya kaunti.

 

Katika taarifa Jumatatu, mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema saini 31,829 zililitoka kwa wafuasi na habari zisizo kamili; 456,079 kutoka kwa wale wanaoonekana zaidi ya mara moja; 7,549 kutoka kwa wale walio na rekodi lakini hawana saini; 668,578 ambao hawakuwa kwenye daftari la wapiga kura na mmoja ambaye alipinga.

Uhakiki ulikamilishwa mnamo Februari 18.

Kaunti ambazo zimepitisha Mswada huo ni Samburu, Nairobi, Vihiga, Laikipia, Kisii, Siaya, Kisumu, Kajiado, Pokot Magharibi, Busia, Trans Nzoia na Homa Bay.

Kufikia sasa, ni Kaunti ya Baringo tu ambayo imekataa Mswada huo.

View Comments