In Summary

•Kuria medai kuwa anaumizwa sana na hali duni ya barabara inayoelekea Mukurwe Wa Nyagathanga ambako kulikuwa makazi yake Gikuyu na Mumbi.

•Ametangaza kufanya mkutano wa kutia saini mkataba wam kumtaka Macharia kutengeneza barabara hiyo karibu na Mukurwe Wa Nyagathanga ambako ibada ya kumtawaza Muturi itakuwa inaendelea siku ile.

Mbunge wa Gatundu ya Kusini, Moses Kuria ameoneka kukeji ibada ya kutawazwa kwake spika wa Bunge la kitaifa kuwa msemaji wa eneo la Mt Kenya.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook, Kuria amedai kuwa anaumizwa sana na hali duni ya barabara inayoelekea Mukurwe Wa Nyagathanga ambako kulikuwa makazi yake Gikuyu na Mumbi.

Kutokana na umuhimu wa wa hekalu hiyo, tumekuwa tukiagiza barabara inayoelekea huko iwekwe lami. Tutatia saini lalamiko la kumtaka waziri James Macharia anayetoka eneo hilo kutengeneza barabara ile” Kuria aliandika.

ujumbe wa kuria
Image: Hisani
Aliendelea kwa kusema kuwa wangeshiriki mkutano wa kutia saini mkataba huo siku ya Jumamosi katika eneo la Gakuyu lililomo karibu na Mukurwe Wa Nyagathanga ambamo ibada ya kumtawaza Muturi itakuwa inaendelea siku ile.
View Comments