Image: HISANI

Pande zote mbili za mapigano na wafuasi wao zasherehekea zikidai ushindi kufuatia kusitishwa kwa mapigano. Kundi la Shia la Hezbollah huko Lebanon limesifu upande wa Palestina kwa "makabiliano ya kishujaa".

"Upinzani wa Palestina... ulianzisha sheria mpya ammbazo zitakuwa mwongozo katika kufikiwa kwa ushindi mkubwa zaidi," kundi la Hezbollah limesema.

Limeongeza kuwa "ushindi... utakuwa na mkakati muhimu sana, athari za kisiasa na kitamaduni katika hatma ya migogoro eneo hilo."

Hezbollah, ambalo limejihami na linalofadhiliwa na mahasimu wa Israel la Iran, ndio kikosi chenye nguvu kubwa huko Lebanon pamoja na jeshi la Lebanon na kwa pamoja na washirika wake wakisiasa, ni kikosi chenye ushawishi mkubwa serikalini.

Kiongozi wa Hamas Ismail Haniya ametangaza ushindi pia na kusema mapambano haya amedhihirisha kuwa "mazungumzo hayawezi kuwa suluhu."

Haniya ameahidi, baada ya ushindi huo wa kijeshi na kisiasa, kundi hilo pamoja na wanaharakati wengine watajitoa kuijenga upya tena Gaza.

Bwana Netanyahu amekuwa akielezea lengo la Israel katika kuanzisha operesheni yake huko Gaza wiki jana. Amesema "lilikuwa pigo kubwa dhidi ya makundi ya kigaidi na imefanikiwa kurejesha utulivu''.

"Sio kila kitu kilichotokea kinajulikana na umma hadi kufikia sasa, sio Hamas, lakini kuna mafanikio makubwa ambayo yatawekwa wazi kadiri muda unavyokwenda," amesema, kulingana na gazeti la Jerusalem Post.

Rais Netanyahu
Image: HISANI
Soma zaidi HAPA
View Comments