In Summary
  • Watu 2 wameaga dunia kufuatia ajali ya barabara kuu ya Mombasa huko Athi River
Watu 2 wameaga dunia kufuatia ajali ya barabara kuu ya Mombasa huko Athi River
Image: George Owiti

HABARI NA GEORGE OWITI;

Watu wawili wamefariki siku ya Jumatatu huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya katika ajali ya barabarani katika barabara kuu ya Nairobi - Mombasa eneo la Still Plant huko Athi River.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Athi River Anderson Njagi alisema wawili hao walifariki papo hapo kwenye ajali iliyohusisha lori na trela mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi.

Njagi alisema lori hilo lilikuwa likisafiri kutoka Nairobi kuelekea Mombasa, huku trela likielekea upande tofauti na kusababisha kugongana.

Alimlaumu dereva wa lori kwa ajali hiyo.

"Dereva hakufuata maagizo ya kugeuza. Aliendelea dhidi ya trafiki. Kwa hiyo, kulikuwa na mgongano wa  ana kwa ana. Dereva wa lori alifariki papo hapo na mvulana wake wa zamu, abiria alijeruhiwa vibaya na amekimbizwa katika Hospitali ya Jamii ya Shalom huko Athi River pamoja na dereva wa trela ambaye alivunjika mguu,” Njagi alisema.

Miili hiyo ilitolewa hadi katika Hospitali ya Jamii ya Shalom huku magari yakikokotwa hadi kituo cha polisi cha Athi River yakisubiri kukaguliwa.

Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

Mkuu huyo wa polisi aliwaonya madereva dhidi ya kukiuka sheria za trafiki wanapokuwa barabarani.

“Madereva wafuate alama na maelekezo ya barabarani. Dereva huyo hakufuata maagizo ya kuelekeza njia," Njagi alisema.

Njagi pia aliwatahadharisha madereva hasa wale wanaoendesha magari makubwa ya kibiashara ya masafa marefu dhidi ya kuendesha huku wakiwa wamechoka.

“Madereva wasimame na kupumzika wakiwa wamechoka badala ya kuendesha na kusababisha ajali. Ninatoa wito kwa madereva wa malori hasa katika barabara ya Mombasa kuwa waangalifu wakati huu ambao barabara hiyo inajengwa,” Njagi alisema.

 

Watu 2 wameaga dunia kufuatia ajali ya barabara kuu ya Mombasa huko Athi River
Image: George Owiti
View Comments