In Summary
  • Lakini katika taarifa siku ya Jumatatu, polisi walisema kuwa mwanamke huyo hakutekwa nyara
Crime Scene

Polisi wanazingatia mashtaka makubwa dhidi ya dereva aliyehatarisha maisha ya mpenzi wake na watumiaji wengine wa barabara.

Polisi walikuwa wakijibu video ambayo ilikuwa imesambazwa na mwanamke akipiga kelele kwenye gari la aina ya ProboxKBJ 835Z, iliyokuwa inaendeshwa kwa kasi, kando ua barabara ya Thika.

Katika video hiyo iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, inasemekana mwanamke huyo ambaye hakutambuliwa alichukuliwa kutoka Chuo Kikuu cha Kenyatta na kuwekwa  kwenye Probox kabla ya kuanza kwa mwendo wa kasi.

Juhudi za kulisimamisha gari hilo hazikufua dafu kwani dereva aliondoka kwa kasi.

Lakini katika taarifa siku ya Jumatatu, polisi walisema kuwa mwanamke huyo hakutekwa nyara.

"Tangu imejulikana kuwa tukio hilo linahusisha wanandoa (mpenzi na rafiki wa kike) ambao walitofautiana baada ya matembezi ya kijamii ndani ya jiji," polisi walisema.

Polisi walisema kuwa mwanamke huyo alitaka kushuka na kwenda nyumbani, huku mpenziwe akisisitiza kukaa pamoja jioni hiyo.

"Wakati wa mzozo huo, mwanachama wa umma alichukua klipu ambayo ilisambazwa mtandaoni," polisi walisema.

"Jana baada ya maridhiano, wanandoa hao waliripoti kwa polisi ili kuondoa kisa hicho kutoka kwa hatua ya polisi."

Tukio hilo ambalo watu wengi walidhania kuwa la kutekwa nyara linachunguzwa na polisi wa Kasarani.

 

 

 

 

 

View Comments