logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mauaji ya Zawahiri ‘yatahitimisha kipindi cha majonzi’ kwa waathiriwa wa Kenya

Mashambulio ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania ni mojawapo ya mashambulizi ya awali ya al-Qaeda.

image
na Radio Jambo

Makala02 August 2022 - 11:10

Muhtasari


•Mauaji ya Ayman al-Zawahiri ‘yatahitimisha kipindi cha majonzi’ kwa wahasiriwa wa Kenya waliojeruhiwa katika shambulio la al-Qaeda kwenye ubalozi wa Marekani, Nairobi.

•Douglas Sidialo, msemaji wa chama cha wahasiriwa wa Kenya, alitaja mauaji ya al-Zawahiri kama ‘’tendo la Mungu’’.

alipoteza uwezo wake wa kuona katika shambulio la ubalozi wa Marekani mjini Nairobi mwaka wa 1998

Mauaji ya Ayman al-Zawahiri ‘yatahitimisha kipindi cha majonzi’ kwa wahasiriwa wa Kenya waliojeruhiwa katika shambulio la al-Qaeda kwenye ubalozi wa Marekani huko Nairobi miaka 24 iliyopita.

Mashambulio hayo mawili dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania ni mojawapo ya mashambulizi ya awali ya al-Qaeda na yalisababisha vifo vya zaidi ya 200 siku hiyo hiyo.

Douglas Sidialo, msemaji wa chama cha wahasiriwa wa Kenya, alitaja mauaji ya al-Zawahiri kama ‘’tendo la Mungu’’.

Aliambia kipindi cha Newsday cha BBC: ‘’Ni vizuri imetokea - kwamba wanawajibisha wale waliohusika na vitendo hivi viovu na vya kinyama.’’

Lakini alilalamika kuwa hasara kwa familia za Kenya za wahasiriwa au wale waliojeruhiwa katika shambulio hilo hazijalipwa.

Haya yanajiri licha ya ahadi ya Joe Biden mnamo mwaka 2010, alipokuwa makamu wa rais, ya kuangazia swala la fidia alipozuru Nairobi.

‘’Najua raia wa Marekani, wanakandarasi na wafanyakazi wa ubalozi huo walilipwa... lakini sisi kama Wakenya hatujawahi kuzingatiwa katika kulipwa fidia.’’

Na hii imekuwa maumivu.

‘’Najua raia wa Marekani, wanakandarasi na wafanyakazi wa ubalozi huo walilipwa fidia... lakini sisi kama Wakenya hatujawahi kufikiriwa kulipwa fidia.Na hii imekuwa maumivu.’’

‘’ Wamarekani wanapaswa kujitokeza na kuhakikisha kwamba sisi waathiriwa wa Kenya tunalipwa’’.

Lazima tuhakikishe haki za binadamu za Wakenya zinashughulikiwa sawa na Wamarekani.

‘’Wamarekani wanapaswa kujitokeza na kuhakikisha kwamba sisi wahasiriwa wa Kenya tunalipwa. Lazima tuhakikishe haki za binadamu za Wakenya zinashughulikiwa sawa na Wamarekani.’’


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved