In Summary

• Rais Kenyatta aliwataka wasaga nafaka kuweka tofauti zao kando na kupunguza bei kama njia moja ya kumjali mwananchi wa kawaida anayeumia.

• Haya yanakuja siku mbili tu baada ya serikali kutangaza kupunguzwa kwa bei kutoka 230 hadi 100 lakini wasaga nafaka wakagomea amri hiyo.

Rais Uhuru Kenyatta wakati akihutubia taifa akitaka wasaga nafaka kukubali kupunguza bei ya unga wa mahindi hadi shilingi 100 kwa pakiti ya kilo 2.
Image: Maktaba

Rais Uhuru Kenyatta ametoa agizo la mwisho kuhusu bei ya unga wa mahindi huku kukiwa na hali ya taharuki ambayo imesababisha gharama hiyo kupita kiwango cha Ksh200.

Akiongea katika Ikulu mnamo Jumatano, Julai 20, Uhuru aliagiza kwamba serikali itatoa ruzuku ambayo itapunguza gharama ya unga wa mahindi hadi Ksh 100 kwa pakiti ya 2Kg mara moja.

Rais pia alisitisha Ada ya Tangazo la Kuagiza (IDF) iliyowekwa kwa mahindi yanayoagizwa kutoka nje pamoja na ushuru wa maendeleo ya mafuta kwa usafirishaji wa mahindi hayo.

Rais alizungumza na washikadau akiwemo Waziri wa Kilimo Peter Munya na wasaga mahindi, ambao walikubali kufuata agizo la serikali.

Alidokeza kuwa mnamo Julai 2012, bei ya pakiti ya kilo 2 ya Unga ilipanda kutoka Ksh70 hadi Ksh130. Mnamo Mei 2017, bei ilipanda hadi Ksh189 na kwa sasa bei imepanda tena hadi Ksh205.

"Kila uchaguzi katika nchi yetu umevutia mzozo wa Unga na wakati fulani unaonekana kutengenezwa. Kuna mwelekeo dhahiri kati ya jinsi bei ya Unga inavyopanda na kupanda kwa kasi wakati wa uchaguzi," Uhuru alisema.

Aliendelea kusema kuwa kudorora kwa mazao, uvamizi wa nzige, changamoto za vifaa kutokana na COVID-19 na vita vilivyopo nchini Ukraine vimesukuma gharama ya vyakula vya kimsingi zaidi ya vikundi vilivyo hatarini.

Uhuru alitoa wito kwa wasagaji hao kuweka kando tofauti zao na kuzingatia mwananchi ambaye anaumizwa na bei ya Unga ya sasa.

"Wakati huu unahitaji tuchukue hatua kwa umoja ili kuwaokoa wanyonge katika jamii yetu, tunapoendelea kutafuta njia endelevu za kukabiliana na hali hii inayoibuka," rais Kenyatta alisema.

Hapo awali, Wazira Munya aliingia makubaliano na wasagaji juu ya ruzuku sawa lakini wasagaji walisita kutia saini mkataba huo hadi serikali ilipoonyesha kujitolea.

Bei ya unga wa mahindi ilikuwa imepanda juu zaidi kutokana na uhaba mkubwa wa hisa za humu nchini uliosababishwa na ukame unaoendelea katika pembe ya Afrika miongoni mwa maeneo mengine.

Waziri Munya alifichua kwamba kuagiza nafaka hiyo kutoka nje ni ghali sana kwa wasagaji wa humu nchini jambo ambalo huenda likawalazimu baadhi yao kusimamisha uzalishaji au kuongeza bei.

View Comments