logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vipigo vya aibu kwa vilabu vikubwa vya EPL

Kipigo cha Man United na Liverpool kuathiri mbio zao za kuwania ubingwa wa EPL.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 March 2023 - 12:21

Muhtasari


•Mashetani Wekundu walipewa kipigo cha aibu na Liverpool kwenye Uwanja wa Anfield siku ya Jumapili.

•Man United waliwatandika Arsenal mabao nane kwa mbili mwaka wa 2011.

Mashetani Wekundu walipata kipigo cha aibu kwenye Uwanja wa Anfield siku ya Jumapili huku mabao saba yakipita wavuni bila wao kupata nafasi hata ya kufunga angalau bao moja la kufuta machozi.

Kipigo hicho kuliwaacha katika nafasi ya tatu wakiwa na alama 49 na kuathiri mbio zao za kuwania ubingwa wa EPL.

Washambulizi Cody Gakpo, Mohammed Salah na Darwin Nunez walifunga mabao mawili kila mmoja wakati wa mchuano huo wa kusisimua huku Mbrazil Roberto Firmino ambaye aliingia kama mchezaji wa akiba katika kipindi cha pili akifunga ushindi wa kihistoria wa Liverpool kwa bao maalum.

Ushindi wa Jumapili jioni ndio ushindi mkubwa zaidi kwa Liverpool dhidi ya Manchester United katika historia ya EPL.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved