Image: GETTY IMAGES

Wanawake wamepigwa marufuku kushiriki katika vipindi vya runinga nchini Afghanistan katika sheria mpya iliowekwa na serikali ya Taliban.

Waandishi wa kike na watangazaji pia wametakiwa kuvalia hijabu katika runinga , ijapokuwa maelezo hayo mapya hayasemi wanafaa kujifunika kwa namna gani.

Waandishi wa habari wanasema baadhi ya sheria hazieleweki na zinapaswa kutafsiriwa.

Taliban lilichukua madaraka nchini Afghnistan katikati ya mwezi Agosti na wengi wanaohofia wanaweka sheri kali.

Kundi hilo la wapiganaji wa Kiislamu, ambalo lilichukua udhibti wa taifa hilo kufuatia kuondoka kwa vikosi vya Marekani na washirika wake pia viliwataka wasichana na wanawake kutoenda shule.

Wakati wa utawala wao miaka ya tisini , wanawake walipigwa marufuku kupata elimu na kufanyakazi.

Maelezo ya hivi karibuni ya Taliban , ambayo yametolewa na runinga ya Afghanistan yalishirikisha sharia nane.

Kupiga maraufuku filamu zinazofikiriwa kwenda kinyume na sheria ya Kiislamu huku picha za wanaume wanaonesha miili yao pia ikipigwa marufuku. Vipindi vya kuchekesha na vya burudani vinavyotusi dini ama ambavyo vinaweza kuonekana kwenda kinyume na mafunzo ya dini pia havitakiwi.

View Comments