logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vijana Zimbabwe watumia taulo za kike na nepi za mkojo za watoto kama 'kilevi'

Kemikali hiyo ndiyo inayotumika kunyonya damu ya hedhi kwenye pedi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri27 April 2022 - 11:58

Muhtasari


• Wanapata dutu nyeupe au kemikali inayojulikana kama sodium polyacrylate - kutoka kwa bidhaa hizi na kuichemsha.

Baadhi ya vijana nchini Zimbabwe wanaripotiwa kuchukua kemikali zinazotumika kwenye nepi na taulo za kike 'pedi' na kuzitumia kama kilevi cha bei nafuu.

Wameiambia Al Jazeera kwamba wanapata dutu nyeupe au kemikali inayojulikana kama sodium polyacrylate - kutoka kwa bidhaa hizi na kuichemsha. "Baada ya kuchemsha, huunda dutu ya kijivu na tunakunywa mchanganyiko huo," kijana mwenye umri wa miaka 19 aliiambia Al Jazeera.

Kemikali hiyo ndiyo inayotumika kunyonya damu ya hedhi kwenye taulo za kike 'pedi' na mkojo kwenye nepi za watoto 'diapers'. Inayeyuka mara moja inapochemshwa.

Matumizi mabaya ya dawa za kulevya na utumiaji wa njia mbadala za vijana kujiinua inatupiwa lawama kutokana na kukosekana kwa mitandao ya usalama wa kijamii nchini Zimbabwe huku kukiwa na uchumi duni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved