logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake wapigwa marufuku kuonyesha nyuso zao kwenye TV Afghanistan

Hapo awali wanawake wote kuamriwa kuficha nyuso zao wakiwa hadharani,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri22 May 2022 - 04:44

Muhtasari


•Uamuzi huo unakuja wiki mbili baada ya wanawake wote kuamriwa kuficha nyuso zao wakiwa hadharani, au vinginevyo kupewa adhabu.

Watangazaji wanawake Afghanistan wanapaswa kuvaa vazi la namna hii wakiwa wanatangaza

Kundi la Taliban limewaamuru watangazaji wa televisheni wa kike wa Afghanistan na wanawake wengine kwenye kufunika nyuso zao wakiwa hewani kwenye vipindi vyaTelevisheni.

Vyombo vya habari viliambiwa kuhusu agizo hilo siku ya Jumatano, msemaji wa polisi wa kidini aliambia BBC. Uamuzi huo unakuja wiki mbili baada ya wanawake wote kuamriwa kuficha nyuso zao wakiwa hadharani, au vinginevyo kupewa adhabu.

Vikwazo vinaimarishwa dhidi ya wanawake - wakipigwa marufuku kusafiri bila kuambatana na mwanaume na wasichana marufku kuhudhuria masomo katika shule za sekondafri.

Getty ImagesCopyright: Getty ImagesWatangazaji wanawake Afghanistan wanapaswa kuvaa vazi la namna hii wakiwa wanatangazaImage caption: Watangazaji wanawake Afghanistan wanapaswa kuvaa vazi la namna hii wakiwa wanatangaza

Mwanahabari mmoja wa kike wa Afghanistan anayefanya kazi katika kituo cha televisheni cha mjini Kabul, ambaye hakutaka kutajwa jina, alisema alishtuka kusikia taarifa hiyo. "Wanatuwekea shinikizo zisizo za moja kwa moja kutuzuia kutangaza kwenye TV," aliambia BBC. "Ninawezaje kusoma habari nikiwa nimeziba mdomo? Sijui la kufanya sasa - lazima nifanye kazi, mimi ndiye mlezi wa familia yangu."

Amri hiyo mpya itaanza kutekelezwa kuanzia tarehe 21 Mei, shirika la habari la Reuters liliripoti, likimnukuu msemaji wa Wizara ya Taliban ya Kuzuia Umakamu na Kukuza Utu wema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved