logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mlipuko mkubwa waua 40 na kujeruhi mamia ya watu Bangladesh

Wengi wa waliojeruhiwa wanaripotiwa kuwa katika hali mbaya

image
na Radio Jambo

Makala05 June 2022 - 12:14

Muhtasari


•Chanzo cha moto huo hakijajulikana, lakini inadhaniwa kemikali zilihifadhiwa katika baadhi ya makontena.

•Wengi wa waliojeruhiwa wanaripotiwa kuwa katika hali mbaya huku majeraha ya moto yakichukua asilimia 60 hadi 90 ya miili yao.

Moto na mlipuko mkubwa umesababisha vifo vya takriban watu 40 baada ya vifo 8 kuongezeka na mamia ya wengine kujeruhiwa kwenye ghala moja lililoko karibu na mji wa Chittagong, Bangladesh.

Mamia ya watu walifika kukabiliana na moto huo wakati makontena kadhaa yalilipuka katika eneo la Sitakunda. Chanzo cha moto huo hakijajulikana, lakini inadhaniwa kemikali zilihifadhiwa katika baadhi ya makontena hayo. Hospitali katika eneo hilo zimezidiwa na zimeomba kuchangia damu. Wengi wa waliojeruhiwa wanaripotiwa kuwa katika hali mbaya huku majeraha ya moto yakichukua asilimia 60 hadi 90 ya miili yao.

"Mlipuko huo ulinirusha umbali wa mita 10 kutoka mahali nilipokuwa nimesimama. Mikono na miguu yangu imeungua," dereva wa lori Tofael Ahmed aliambia shirika la habari la AFP.

Mhudumu mwingine wa kujitolea aliambia shirika hilo kuwa ameona miili zaidi ndani ya eneo lililoathiriwa na moto huo. Wazima moto kadhaa ni miongoni mwa waliouawa na kujeruhiwa. Bohari hiyo ilikuwa na nguo za mamilioni ya dola zilizokuwa zikisubiri kusafirishwa kwa wauzaji reja reja wa nchi za Magharibi, kulingana na afisa wa serikali ya eneo hilo. Bangladesh ni muuzaji mkuu wa nguo kwa nchi za Magharibi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved