logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 230 wauawa Sudan Kusini kwenye mzozo wa mifugo

Mapigano hayo yanajiri wakati Sudan Kusini inaadhimisha miaka 11 ya uhuru.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 July 2022 - 12:59

Muhtasari


• Mamlaka nchini Sudan Kusini zimesema zaidi ya watu 230 wameuawa katika muda wa wiki mbili zilizopita katika mapigano ya kikabila kusini mwa nchi hiyo.

Mamlaka nchini Sudan Kusini zimesema zaidi ya watu 230 wameuawa katika muda wa wiki mbili zilizopita katika mapigano ya kikabila kusini mwa nchi hiyo.

Mzozo kuhusu ng'ombe na mashamba ya malisho ulitokea katika jimbo la Ikweta Mashariki kuanzia mapema mwezi huu. Mauaji hayo yametokea katika kaunti ya Kapoeta Kaskazini ambapo jamii hasimu zilipambana kufuatia uvamizi wa mifugo katika mojawapo ya vijiji hivyo.

Waliouawa ni pamoja na chifu wa eneo hilo ambaye alipigwa risasi. Gavana wa jimbo hilo amelaani mauaji hayo na kuiomba serikali kutuma haraka vikosi vya usalama katika eneo hilo ili kusaidia kurejesha hali ya utulivu.

Ilikuja wakati Sudan Kusini inaadhimisha miaka 11 ya uhuru. Umoja wa Mataifa umeonya kuwa nchi hiyo iko katika hatari ya kurejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na mapigano baina ya jamii ambayo yamesababisha mamilioni ya watu kuyahama makazi yao.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved