In Summary

•Taiwan imesema kwamba meli na ndege "nyingi" za China zimevuka mstari wa kati wa Taiwan.

Ndege za kivita za China zilikuwa zikiruka juu ya kisiwa cha Pingtan cha bara - ambacho kiko katika Mlango-Bahari wa Taiwan kutoka kaskazini mwa Taiwan na ni mojawapo ya maeneo ya karibu zaidi katika bara na kisiwa hicho.

Picha zinaonyesha ndege hizo zikiwa na makombora.

Watalii katika kisiwa hicho walikuwa wakiziona ndege hizo kwa kutumia darubini.

China pia ilirusha makombora juu ya Taiwan kutoka Kisiwa cha Pingtan siku ya Alhamisi.

Kama tulivyoripoti hapo awali, wizara ya ulinzi ya Taiwan imesema leo kwamba meli na ndege "nyingi" za China zimevuka mstari wa kati wa Taiwan Strait kwa siku ya pili mfululizo.

Chanzo cha Taiwan kilichofahamishwa kuhusu suala hilo sasa kimeiambia Reuters kwamba takriban meli 10 za jeshi la wanamaji la China zilivuka mstari wa mpaka na kubaki katika eneo hilo siku ya Ijumaa asubuhi, na takriban ndege 20 za kijeshi za China pia zilivuka eneo hilo kwa muda mfupi.

Meli za jeshi la majini za Taiwan ziko karibu kufuatilia shughuli za jeshi la wanamaji la China, chanzo kiliongeza.

Mstari wa ‘kati’ni mstari usio rasmi wa kugawanya mpaka kati ya China bara na Taiwan.

China yamuwekea vikwazo PelosI

China imetangaza kumuwekea vikwazo Spika wa Marekani Nancy Pelosi na familia yake ya karibu katika ziara yake nchini Taiwan.

Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi alisema kuwa Pelosi "ameingilia sana mambo ya ndani ya China, ameharibu vibaya mamlaka na ukamilifu wa ardhi ya China, akapuuza pakubwa kanuni ya kuwa na China moja, na kutishia pakubwa amani na utulivu katika Mlango-Bahari wa Taiwan", kulingana na taarifa.

China inaiona Taiwan kama jimbo lililojitenga ambalo lazima liunganishwe na bara, kwa nguvu ikiwa italazimu

View Comments