logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Urusi na Ukraine: Mtoto asikika akilia 'kwaheri baba' huku babake raia wa Urusi akienda vitani Ukraine

Rais Vladimir Putin aliamuru kuwasajili Warusi zaidi ya 300,000 wenye uzoefu wa kijeshi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 September 2022 - 08:05

Muhtasari


• Urusi imeanza kutekeleza mipango ya kuwaita askari wa akiba kupigana nchini Ukraine baada ya kukabiliwa vilivyo na wanajeshi wa Ukraine.

Mtoto anasikika akilia huku akimuaga baba yake katika video iliyosambazwa kwenye Telegram. Video hiyo inaonyesha wanaume wa Urusi wanaopanda mabasi kwenda kupigana vitani.

Mwandishi wa BBC Will Vernon aliweza kuthibitisha kanda hiyo baada ya kuzungumza na wenyeji wa Staryi Oskol katika Mkoa wa Belgorod, akiwemo mwanamke mmoja ambaye alikuwepo wakati video hiyo iliporekodiwa. Video hiyo imesambazwa katika programu ya kijamii ya Telegraph.

Urusi imeanza kutekeleza mipango ya kuwaita askari wa akiba kupigana nchini Ukraine baada ya kukabiliwa vilivyo na wanajeshi wa Ukraine.

Rais Vladimir Putin aliamuru kuwasajili Warusi zaidi ya 300,000 wenye uzoefu wa kijeshi, na hivyo kuzua maandamano nchini humo siku ya Jumatano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved